Description
Dini ni Nini?
Dini ni kitendo kinachotokana na imani fulani, hasa imani katika mambo ya rohoni. Pale mtu anapoamini uwepo wa Mungu, shetani, au chochote kisichoonekana na kinachoabudiwa, dini inazaliwa. Hapo ndipo utaona mtu anajiwekea miiko, utaratibu, au ustaarabu fulani. Kwa mfano, wanaoamini Buddha wana taratibu za kufuata ili kumwabudu mungu wao; wanavaa mavazi fulani, wanapitia madarasa fulani, wanaishi maisha ya kujinyima, hawashirikiani na jamii fulani, wanafunga, au hawali vyakula fulani. Hiyo ndiyo inayoitwa dini.
Dini katika Ukristo
Vivyo hivyo, katika Ukristo, mtu yeyote mwenye imani ya kweli katika Yesu Kristo lazima atakuwa na kiwango fulani cha dini ndani yake. Mkristo atajijengea utaratibu wa kuomba kila siku, kufunga mara kwa mara, kuhudhuria ibada kanisani, kutoa sadaka, na kuwasaidia wengine. Biblia inasema katika Yakobo 1:26-27, hivyo dini ya kweli ni ile iliyoonyeshwa kwenye mstari wa 27. Lakini dini haimpi mtu tiketi ya moja kwa moja kwenda mbinguni, bali inamrahishia tu njia. Tofauti na imani nyingine ambazo kushika dini ndiko kuokoka, katika Ukristo usipomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zako katika damu yake, huwezi kwenda mbinguni. Unaweza kufunga, lakini kama maisha yako yapo mbali na Kristo, utakwenda kuzimu. Unaweza kuhudhuria ibada kila siku na kushika mambo yote unayoambiwa kanisani, lakini kama hauna Roho Mtakatifu, ni bure. Tofauti na dini nyingine ambazo kwazo dini ni kitu cha kujivunia, katika Ukristo, dini ni chombo cha kumuelekea Mungu.
Imani ya Kweli ni Ipi?
Kwa ufupi, dini ni njema ikiwa imeambatana na imani ya kweli. Ni sawa na shule yenye mazingira mazuri na walimu wazuri, ambayo inamjengea mwanafunzi mazingira mazuri ya kufaulu mitihani. Lakini shule pekee, hata kama ina jengo zuri au inajulikana, haimfanyi mwanafunzi afaulu mitihani kama hana bidii yake binafsi. Baada ya kujua dini ni nini na dini ya ukweli ni ipi, ni vizuri kujua imani ya kweli ni ipi. Imani ya kweli ni ile iliyopo katika kumwamini Yesu Kristo kama mwana wa Mungu na aliyetumwa kuja kuwaokoa wanadamu. Hiyo ndiyo imani ya kweli. Imani nyingine tofauti na hiyo ni imani ya uongo na inayopotosha na kupeleka watu mautini. Katika somo hili, tutajadili kwa undani dini 12 kubwa duniani.
Reviews
There are no reviews yet.